Tengeneza Hesabu za Biashara

by Ali Mwambola

Product Description:

Hiki kitabu kimechapishwa kuwasaidia wajasiriamali ambao hawana elimu ya uhasibu

Sasa hivi ninafanya kazi kama Business Consultant, ninayetoa ushauri kwa wajasiriamali na wafanyabiashara mbali mbali

Nimejaribu kuwauliza wafanyabiashara wengi na wajasiriamali, kama biashara zao zinapata faida au hasara

Nimesikitika baada ya kufahamu kuwa wengi wao, hawafahamu kama wanapata faida au hasara, kwa sababu hawatengenezi hesabu za biashara zao

Sababu wanayotoa ya kutotengeneza hesabu za biashara zao, ni kuwa, hawana uwezo wa kifedha wa kuajiri wahasibu

Kutokana na hali hiyo, nimeamua kusaidia kupata ufumbuzi wa hili jambo, kwa kuchapisha hiki kitabu

Nimeandika hiki kitabu kwa kutumia lugha nyepesi ya kihasibu, kusudi nieleweke na wengi ambao hawana elimu ya uhasibu

Majarajio yangu ni kuwa, nitakuwa nimewasaidia wajasiriamali wengi kuweza kutengeneza hesabu za biashara zao wenyewe