Mtaji wa Kuanzisha Biashara

Ujasiriamali

by Ali Mwambola

Product Description:

Napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru walio saidia kufanikisha uchapishaji wa hiki kitabu. Kitabu hiki kimetayarishwa kutokana na maswali mengi ambayo nimekuwa napata kutoka kwa wajasiriamali kuhusu mtaji wa kuanzisha biashara

Wajasiriamali wengi wanadhani kuwa kuna kiasi maalum cha fedha ambacho kinatosha kuanzisha biashara za aina mbali mbali

Mfano wa maswali ambayo nimekuwa napata ni kama ifuatavyo:

"Kiasi gani cha mtaji kinatosha kuanzisha biashara ya stationery"

"Mimi ninazo shs 1,500,000 ambazo ninataka nianzishe salon, naomba ushauri iwapo hizo fedha zinatosha"

"Naomba ushauri jinsi ya kupata mtaji kutoka bank wa kuanzisha garage ya magari"

"Shilingi ngapi zinatosha kuanzisha biashara ya unga wa sembe?"

Ukweli wa mambo ni kuwa, hakuna kiasi maalum cha fedha ambacho kinaweza kutumika kama mtaji wa kuanzisha biashara

Mjasiriamali mmoja anaweza kuanzisha duka la vipodozi kwa shs 5,000,000 na   mwengine anaweza kutumia shs 50,000,000 kuanzisha biashara ya vipodozi

Unachotakiwa kufahamu ni kuwa, kuna vigezo maalum ambavyo hutumika wakati wa kukadiria ukubwa wa mtaji ambao una tosha kuanzisha biashara

Hiki kitabu kinaeleza mambo mbali mbali muhimu kuhusu mtaji wa biashara pamoja na maelezo ya jinsi ya kukadiria mtaji wa biashara na wapi unaweza kupata fedha za mtaji

 

Ali Mwambola

Dar es Salaam